Tuesday, April 22, 2014

NEYMAR ANAIWAZA ZAIDI BARCELONA KULIKO KOMBE LA DUNIA - BABA.

BABA wa mshambuliaji nyota wa Barcelona, Neymar amedai kuwa mwanae anafanya jitihada za kurejea uwanjani kuitumikia klabu yake na sio michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika katika majira ya kiangazi. Nyota huyo wa kimataifa wa Brazil kwasasa yuko nje ya uwanjani akijiuguza majeruhi ya mguu wake wa kushoto aliyopata katika fainali ya Kombe la Mfalme, ambapo atakuwa nje kwa kipindi cha wiki nne. Neymara alikaririwa wiki iliyopita akidai kuwa ana malengo ya kuwa fiti kwa ajili ya mchezo wa mwisho wa Barcelona dhidi ya Atletico Madrid, baada ya kukiri kuwa anahofu juu ya matumaini yake ya kucheza Kombe la Dunia. Hata hivyo, baba yake amesema mwanae huyo kwasasa anafikiria kurejea katika kikosi cha kwanza cha Barcelona halafu baada ya hapo ndio atafikiria michuano hiyo itakayofanyika katika ardhi ya nyumbani kwao Brazil. Neymar amefunga mabao 15 katika mechi 40 alizoichezea Barcelona katika mashindano yote msimu huu.

No comments:

Post a Comment