Tuesday, April 29, 2014

SIMEONE AIGWAYA CHELSEA.

MENEJA wa klabu ya Atletico Madrid, Diego Simeone anaamini ushindi wa Chelsea dhidi ya Liverpool bila kuwa na baadhi ya nyota wake unaonyesha jinsi gani wanaweza kuwadhuru wakati watakapokutana katika mchezo wao wa marudiano kesho. Timu hizo mbili zinaingia katika mchezo wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa baada ya kutoka sare ya bila ya kufungana Jumanne iliyopita. Simeone amesema ni wazi Chelsea wana timu kubwa kwasababu wameshinda pamoja na kufanya mabadiliko mengi, hiyo inamaanisha watakwenda kucheza na timu yenye nguvu. Atletico wataingia kutafuta nafasi ya kucheza fainali ya kwanza ya michuano hiyo toka mwaka 1974 wakati walifungwa na Bayern mabao 4-0 huko Heysel.

No comments:

Post a Comment