Tuesday, April 29, 2014

WENGER AKIRI MAJERUHI NDIO CHANZO CHA TIMU YAKE KUPOROMOKA.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amekiri kuwa majeruhi ya mara kwa mara kwa nyota wake ndio yaliyochangia kwa kiasi kikubwa kushindwa mbio za kugombea taji la Ligi Kuu. Arsenal ambao jana wameinua matumaini yao ya kumaliza katika nafasi nne za juu katika msimamo wa ligi baada ya kuichabanga mabao 3-0 Newcastle United wamekuwa wakisumbuliwa na majeruhi kwa nyota wake akiwemo Aaron Ramsey ambaye alikuwa nje kwa kipindi kirefu. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Wenger amesema suala la majeruhi limekuwa tatizo kubwa kwake kwani aliwapoteza wachezaji wake nyota katika kipindi muhimu cha msimu. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa ushindi dhidi yaNewcastle ulikuwa ni muhimu sana kutokana na malengo yao waliyojiwekea. Arsenal sasa wametofautiana na Everton waliopo nafasi ya tano kwa alama nne na wakipata ushindi wa mechi moja watakuwa wamejihakikishia nafasi hiyo.

No comments:

Post a Comment