Sunday, April 20, 2014

WENGER AMTOA HOFU HODGSON KUHUSU HALI YA WILSHERE.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amempa taarifa njema kocha wa timu ya taifa ya Uingereza Roy Hodgson kuwa Jack Wilshere atakuwa fiti kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Juni 12 mwaka huu. Wilshere mwenye umri wa miaka 22 alikuwa amekaa nje ya uwanja toka alipoumia mguu akiitumikia timu ya taifa Machi 5 mwaka huu. Hodgson anatarajia kutaja kikosi cha wachezaji 30 kwa ajili ya michuano hiyo Mei 13 na Wenger amesema amemuhakikishia kuwa Wilshere atakuwa fiti ikifika wakati huo. Wenger amesema nyota huyo ameanza mazoezi kukimbia wiki hii hivyo anadhani baada ya wiki mbioi au tatu atakuwa ameshakuwa fiti tayari kwa kurejea uwanjani. Kupona kwake pia kutamfanya ajumuishwe katika kikosi cha Arsenal kitakachoivaa Hull City katika mchezo wa fainali ya Kombe la FA Mei 17 katika Uwanja wa Wembley.


No comments:

Post a Comment