Thursday, May 29, 2014

MBEYA CITY WATINGA ROBO NILE BASIN.

TIMU ya Mbeya City imefanikiwa kutinga hatua ya robo fainali ya michuano mipya ya Nile Basin iliyoandaliwa na Baraza la Michezo kwa Nchi za Afrika Mashariki na Kati huko jijini Khartoum, Sudan. Mbeya City ambayo inashiriki michuano yake ya kwanza ya kimataifa ilitinga hatua hiyo baada ya kutoa sare ya bila ya kufungana na timu ya Etincelles ya Rwanda. Katika robo fainali Mbeya City watakwaana na Victoria University ya Uganda huku mechi zingine kwa timu zilizongia hatua hiyo ziliwakutanisha AFC Leopard ya Kenya itachuana na Defence ya Ethiopia. Mechi nyingine itashuhudia Al Merreikh ya Sudan wakichuana na Tchite Academy ya Burundi huku Al-Ahli Shandi wao wakiwa na kibarua kizito cha kupambana na Malakia ya Sudan Kusini.


No comments:

Post a Comment