Thursday, May 29, 2014

MMILIKI WA MAN UNITED AFARIKI DUNIA BAADA YA KUUGUA KWA MUDA MREFU.

KLABU ya Manchester United imekumbwa na simanzi kubwa kufuatia mmiliki wake Malcom Glazer raia wa Marekani kufariki dunia akiwa na umri wa miaka 85. Familia ya Glazer iliinunua klabu hiyo kwa euro milioni 790 Mei mwaka 2005 licha ya kupata pingamizi kali kutoka kwa mashabiki wa klabu hiyo. Chini wa umiliki wake United wanajulikana kwa jina la utani Mashetani Wekundu walifanikiwa kushinda mataji matano ya Ligi Kuu na taji la Klabu Bingwa ya Ulaya mwaka 2008. Watoto wa bilionea huyo Joel na Avram ndiyo waliochukua nafasi ya kuingoza klabu hiyo katika shughuli za kila siku baada ya baba yao kupatwa na ugonjwa wa kiharusi mwaka 2006. Kifo cha Glazer hakitarajiwi kuadhiri umiliki wa United, kwani familia hiyo bado inamiliki asilimia 90 za hisa za klabu hiyo ambazo zimegawanywa sawa kwa watoto wake sita alionao. Huku asilimia 10 inayosalia inamilikiwa na wenye hisa katika soko la hisa la New York.

No comments:

Post a Comment