Sunday, June 22, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: KLOSE AIFIKIA REKODI YA RONALDO.

MSHAMBULIAJI mkongwe wa Ujerumani Miroslav Klose amefikisha idadi sawa ya mabao yaliyofungwa katika michuano ya Kombe la Dunia na aliyekuwa mshambuliaji wa kimataifa wa Brazil Ronaldo de Lima. Klose alifunga bao lake la kumi na tano dhidi ya Ghana katika mechi iliyomalizika kwa sare ya kufungana mabao 2-2. Katika mchezo huo uliokuwa mkali na kusisimua Ujerumani ndio walioanza kupata bao la kuongoza katika kipindi cha pili kabla ya Ghana hawajasawazisha kupitia kwa Andre Ayew na baadae kuongeza la pili kupitia kwa Asamoah Gyan lakini Ujerumani nao wlaiswazisha kupitia kwa mkongwe Klose na kupelekea mchezo huo kumalizika kwa sare hiyo. Wawakilishi wengine wa Afrika Nigeria jana nao walijitoa kumasomaso kwa kuichapa Bosnia-Herzegovina kwa bao 1-0 hivyo kuweka hai matumaini yao ya kusonga mbele katika michuano hiyo kama wakifanikiwa kuifunga Argentina katika mchezo wao wa mwisho.

No comments:

Post a Comment