Sunday, June 22, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: BECKHAM NYUMA YA MWAMKO WA SOKA LA MAREKANI.

HILI ni Kombe la Dunia la kwanza kumkosa David Beckham baada ya kupita zaidi ya miaka 20, hata hivyo kazi yake kubwa aliyoifanya kulitangaza soka nchini Marekani itaonekana baadae leo usiku wakati nchi hiyo itakapoivaa Ureno.

Hakuna shaka kwamba Marekani hivi sasa wameanza kupagawa na mchezo wa soka huku mamilioni wakifuatilia kila hatua na mastaa wa Hollywood wakitumia kurasa zao za mitandao ya kijamii ya twitter kuelezea mchezo wa soka.

Kunatarajiwa kuwa na mshabiki zaidi ya 10,000 wa Marekani huko Manaus katika tiketi 90,000 za Kombe la Dunia zilizouzwa kwa ajili ya michuano hiyo na kufanya kuwa nchi iliyonunua tiketi nyingi zaidi ukiacha wenyeji Brazil katika michuano hiyo.

Katika mchezo huo wa leo zaidi ya mashabiki milioni 20 wa nchi hiyo wanatarajiwa kutizama mchezo huo idadi ambayo inatarajiwa kuizidi ile ya mashabiki waliotizama mchezo wao pendwa wa fainali ya mpira wa kikapu ambapo San Antonio Spurs waliibuka kidedea wiki ijayo.

Kuhama kwa Beckham kutoka klabu ya Real Madrid kwenda Los Angeles Galaxy kumechangia kwa kiasi kikubwa nchi hiyo kupata hamasa ya mchezo huo baada ya utawala wa kipindi kirefu wa michezo ya mpira wa kikapu na baseball.

Mtoto wa kiume wa kocha wa wa Liverpool Kenny Dalglish aitwaye Paul ambaye amekaa Marekani kwa muda wa miaka nane anatoa ushuhuda wa jinsi Beckham alipoinua hamasa ya mchezo soka nchini Marekani katika kipindi cha miaka minne alipokuwepo huko.

Paul amesema Beckham alikuwa zaidi ya mchezaji, kwani wakati anafika Ligi Kuu ya Soka nchini humo maarufu kama MLS ilikuwa na timu 12 pekee lakini msimu ujao wa ligi hiyo unatarajiwa kuwa na timu ya 21.

Nyota mbalimbali akiwemo wa mpira wa kikapu LeBron James ambaye ana zaidi ya watu milioni 13 wanaomfuata katika mtandao wa twitter aliandika katika ukurasa wake kwa kuipongeza nchi hiyo kuanza vyema katika mchezo wa kwanza dhidi ya Ghana.

Nyota wengine walioipongeza nchi hiyo ni Justin Timberlake huku Ikulu ya Marekani nayo iituma salamu zake pamoja na kuwakilishwa na makamu wa rais Joe Badden katika mchezo wa kwanza dhidi ya Ghana.

No comments:

Post a Comment