Sunday, June 22, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: MESSI IS A GENIUS - SABELLA.


KOCHA wa timu ya taifa ya Marekani, Alejandro Sabella amempongeza Lionel Messi kwa ujuzi wake baada ya kufunga bao dakika za majeruhi na kuindosha Iran katika michuano ya Kombe la Dunia. Iran waliichanganya Argentina kwa mchezo wao wa kupaki basi mpaka Messi alipotumia ujuzi binafsi kwa kufunga bao lake la pili katika michuano hiyo. Sabella amesema Iran walifanya maisha kuwa magumu katika mchezo huo lakini anashukuru kwakuwa na mtu mwenye ujuzi ambaye ni Messi aliyefanya mambo yawezekane. Kabla ya michuano hii Messi alikuwa amefunga bao moja katika mechi nane za Kombe la Dunia alizocheza lakini mambo yamebadilika safari hii baada ya kuonyesha uwezo wake katika mechi mbili zilizopita. Sabella amesema wachezaji wake wote walichangia kwa kiasi kikubwa ushindi lakini kwa shuti alilopiga Messi hata kama kungekuwa na magolikipa wawili wasingweza kulizuia.

No comments:

Post a Comment