Sunday, June 22, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: KOLO NA YAYA TOURE WASHINDWA KUMZIKA NDUGU KWA AJILI YA TIMU YA TAIFA.

NDUGU wawili Yaya na Kolo Toure wameamua kubakia na timu yao ya taifa ya Ivory Coast katika michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea nchini Brazil baada ya kifo cha mdogo wao. Ibrahim Toure mwenye umri wa miaka 28 ambaye alikuwa akiugua maradhi ya saratani alifariki dunia Alhamisi iliyopita. Shirikisho la Soka la Ivory Coast lililotoa taarifa hiyo huku wakituma salamu za rambirambi kwa familia ya ndugu hao. Ivory Coast itachuana na Ugiriki katika mchezo wao wa mwisho wa kundi C Jumanne ijayo wakijua kuwa ushindi utawavusha katika hatua inayofuata ya timu 16 bora. Yaya Toure mwenye umri wa miaka 31 anayekipiga katika klabu ya Manchester City amecheza katika mechi zote mbili za Ivory Coast dhidi ya Japana na Colombia wakati beki wa Liverpool Kolo Toure mwenye umri wa miaka 33 bado ameendelea kusugua benchi katika michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment