Monday, June 30, 2014

KOMBE LA DUNIA 2014: ROBBEN AKIRI KUJIRUSHA NA KUOMBA RADHI.

WINGA mahiri wa timu ya taifa ya Uholanzi, Arjen Robben ameomba radhi na kukiri kuwa alijirusha wakati nchi yake ikiitandika Mexico kwa mabao 2-1 katika hatua ya timu 16 bora kwenye michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea nchini Brazil lakini amedai hakujirusha walivyopewa penati. Klaas Jan Hunterlaar alifunga bao la ushindi la Uholanzi kwa penati kwenye muda wa majeruhi baada ya Robben kufanyiwa faulo. Kocha wa timu ya taifa ya Mexico Miguel Herrera alimtuhumu Robben kwa kujirusha mara tatu kwenye mchezo huo lakini winga huyo aliomba radhi kwa kujirusha katika kipindi cha kwanza. Robben aliendelea kudai kuwa penati waliyopewa dakika za mwisho ilikuwa halali kwasababu kweli alifanyiwa madhambi. Robben alifanyiwa faulo na nahodha wa Mexico katika dakika ya 94 ya mchezo huo lakini Herrera anadhani mchezaji huyo wa klabu ya Bayern Munich hakutakiwa kuwepo uwanjani kuweza kuipatia timu yake penati.

No comments:

Post a Comment