Saturday, July 26, 2014

LALLANA KUUKOSA MWANZO WA MSIMU.

KIUNGO mpya wa klabu ya Liverpool, Adam Lallana anatarajiwa kuukosa mwanzo wa msimu wa Ligi Kuu baada ya kuumia mguu wakati akiwa mazoezini. Lallana ambaye aliondoka Southampton mapema mwezi huu kwa ada ya paundi milioni 25 alipata majeruhi hayo wakati wa maandalizi ya msimu mpya huko nchini Marrekani. Kiungo huyo wa kimataifa wa Uingereza bado hajapangwa katika mechi yoyote ya kirafiki ya Liverpool na ingawa haitaji kufanyiwa upasuaji lakini hatarajiwi kuwa fiti kwa ajili ya mchezo wa kwanza wa ligi dhidi ya Southampton utakaochezwa Agosti 17 mwaka huu. Mbali na kukosa mchezo huo Lallana ambaye alikuwemo katika kikosi cha Uingereza kilichoshiriki michuano ya Kombe la Dunia mwaka huu, pia kuna uwezekano wa kuzikosa mechi dhidi ya Manchester City na Tottenham Hotspurs.

No comments:

Post a Comment