Saturday, July 26, 2014

ARSENAL YANASA KINDA LA SOUTHAMPTON.

KLABU ya Arsenal imekubali dili la kumsajili nyota wa klabu ya Southampton Calum Chambers. Mchezaji huyo kinda mwenye umri wa miaka 19 ambaye anaweza kucheza kama beki wa kulia, beki wa kati na nafasi ya kiungo amekuwa akitajwa kama mmoja wa wachezaji bora wanaochipukia katika soka la Uingereza na Arsenal wanakaribia kumsajili kwa ada inayoweza kufikia euro milioni 20. Inaaminika kuwa Chambers tayari amehafanyiwa vipimo vya afya kuelekea kusaini dili hilo ambalo Southampton watalipwa kitita cha paundi milioni 13 kwasasa. Meneja wa klabu ya Liverpool, Brendan Rodgers alikuwa akimtaka kumpeleka kinda huyo Anfield lakini Chambers mwenyewe ameamua kuchagua Arsenal ili aweze kuwa karibu na kocha Arsene Wenger. Chambers anakuwa mchezaji nne kuondoka Southampton katika kipindi hiki cha usajili wa majira ya kiangazi baada ya kuondoka kwa Adam Lallana na Rickie Lambert kwenda Liverpool na Luke Shaw kwenda Manchester United.

No comments:

Post a Comment