Monday, July 28, 2014

PAMOJA NA KUKARIBIA KUMNASA CHAMBERS, WENGER AKIRI DILI HILO NI BAHATI NASIBU.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amethibitisha kuwa klabu hiyo inakaribia kumsajili kinda la Southampton Calum Chambers ingawa amekiri dili hilo ni kama kubahatisha. Arsenal inatarajiwa kutangaza usajili huo wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19 baada ya kufikia makubaliano ya kutoa kitita cha euro milioni 20 cha uhamisho kwenda Emirates. Wenger amesema Chambers anaweza kucheza katika nafasi kama beki wa kati, beki wa kulia na kiungo wa kati hivyo ni mategemeo yake ataleta changamoto katika nafasi hizo kwa wachezaji wenzake. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa pamoja na kuwa Chambers hajacheza mechi nyingi lakini wachezaji wengi wa Uingereza ni ghali hivyo ameamua kubahatisha kwasababu anaweza kuwa mchezaji muhimu siku zijazo. Kinda huyo ambaye ni zao la chipukizi wa wanaopikwa na Southampton anatarajiwa kufuata nyayo za kina Theo Walcott na Alex Oxlade-Chamberlain ambao wote wametokea huko kabla ya kwenda Arsenal.

No comments:

Post a Comment