Monday, July 28, 2014

RENARD BADO APEWA NAFASI YA KUINOA IVORY COAST.

KOCHA Mfaransa Herve Renard ametajwa katika orodha ya majina matatu ya mwisho katika kugombea nafasi ya kuinoa timu ya taifa ya Ivory Coast. Orodha hiyo ilitolewa na Shirikisho la Soka la nchi hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo mshindi wa nafasi hiyo anatarajiwa kutangazwa mwishoni mwa mwezi huu. Renard ambaye aliiongoza timu ya taifa ya Zambia maarufu kama Chipolopolo kushinda kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2012 anakabiliwa na upinzani kutoka kwa Mfaransa mwenzake Frederic Antonetti ambaye alikuwa akiifundisha Rennes na kocha wa zamani wa Sporting Lisbon na Benfica Jose Manuel De Jesus wa Ureno. Watatu hao wanatarajiwa kuhojiwa na kamati ya utendaji ya shirikisho hilo kabla ya uamuzi wa mwisho. Shirikisho hilo limedai kuwa linataka kuteua kocha mpya kabla ya kuanza kwa michuano ya kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika mapema Septemba.

No comments:

Post a Comment