Monday, July 28, 2014

LIGI YA MABINGWA AFRIKA: ZAMALEK YANG'ANG'ANIWA NA TP MAZEMBE.

KLABU ya Zamalek ya Misri imeshindwa kutumia vyema uwanja wake wa nyumbani jijini Alexandria baada ya kung’ang’aniwa sare ya bila kufungana na TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo-DRC katika mchezo wa kundi A wa Ligi ya Mabingwa barani Afrika. Sare hiyo imeiacha Zamalek ikiburuza mkia katika kundi hilo wakiwa na alama nne wakati Mazembe wao waliporomoka kwa nafasi mpaka nafasi ya pili kwa alama saba walizonazo wakifungana na Wacongo wenzao AS Vita ambao waliichapa Al Hilal ya Sudan kwa mabao 2-1 katika mchezo uliochezwa mapema jana jijini Kinsasha. Katika mchezo huo timu zote mbili zilipata nafasi sawa za kuibuka na ushindi lakini walishindwa kuzitumia nafasi zao za kufunga walizopata hizo kuepelekea mchezo huo kumazika kwa sare. Zamalek watabakia nyumbani kwa mchezo wao pili mfululizo pale watakapowakaribisha vinara Vita Agosti 9 mwaka huu wakati Mazembe watawasubiri Al Hilal siku hiyohiyo.

No comments:

Post a Comment