Wednesday, July 30, 2014

SOUTHAMPTON INA CHIPUKIZI WENGI WALIO TAYARI KUCHEZA KIKOSI CHA KWANZA - CHAMBERS.

NYOTA wa zamani wa klabu ya Southampton, Calum Chambers amesema timu hiyo ina wachezaji wengi zaidi chipukizi waliopo tayari kucheza katika kikosi cha kwanza baada ya wachezaji kadhaa wenye majina kuondoka. Chambers mwenye umri wa miaka anayecheza nafasi ya beki wa kulia amekuwa mchezaji wa tano kuondoka Southampton katika kipindi hiki cha usajili wa majira ya kiangazi kwa ada ya paundi milioni 16 kwennda Arsenal. Lakini mchezaji huyo aliyepandishwa katika kikosi cha kwanza msimu uliopita anaamini kuwa wachezaji wengi chipukizi watapata nafasi ya kupandishwa msimu huu. Chambers amesema Southampton wana mfumo mzuri wa timu za vijana hivyo watazalisha wachezaji wengi zaidi. Wachezaji wengine wa Southampton walioondoka kiangazi hiki ni pamoja na Rickie Lambert, Adam Lallana na Dejan Lovren ambao wote wamekwenda Liverpool wakati Luke Shaw yeye amekwenda Manchester United.

No comments:

Post a Comment