Wednesday, July 30, 2014

SABELLA AITEMA ARGENTINA.

VYOMBO vya habari nchini Argentina, vimeripoti kuwa kocha wa timu ya taifa ya nchi hiyo Alejandro Sabella ameamua kujiuzulu. Sabella mwenye umri wa miaka 59 ameisaidia nchi hiyo kutinga fainali ya michuano ya Kombe la Dunia iliyomalizika nchini Brazil mapema mwezi huu. Taarifa zimesema kuwa Sabella alimuambia rais wa Shirikisho la Soka la nchi hiyo Julio Grondona kuwa anaachia nafasi yake hiyo. Argentina inatarajiwa kuanza maandalizi yake ya michuano ya Copa America itakayofanyika nchini Chile kwa kucheza mechi za kirafiki dhidi ya mabingwa wa Kombe la Dunia Ujerumani huko Duesseldorf Septemba 3 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment