Saturday, July 26, 2014

VAN GAAL AWAKOMALIZA WACHEZAJI WAKE KUWASILIANA KWA KIINGEREZA WAWAPO UWANJANI.

KIUNGO aliyevunja rekodi ya usajili katika klabu ya Manchester United, Juan Mata amebainisha meneja mpya Louis van Gaal amewaambia wachezaji wake kuwa wanatakiwa kuwasiliana kwa lugha ya kiingereza. Mata tayari alikuwa ameungana na Ander Herrera wanaotoka nchi moja ambaye alijiunga nao akitokea Atletico Madrid mapema katika kipindi hiki usajili wa kiangazi, hata hivyo wakiwa uwanjani hawataruhusiwa kuzungumza lugha ya kwao Hispania. Hayo sio mabadiliko pekee aliyofanya Van Gaal toka ametua United mapema mwezi huu kwani kocha huyo aliyeingoza vyema Uholanzi kushika nafasi ya tatu katika michuano ya Kombe la Dunia pia amemua kutumia mabeki wake wa pembeni kama mawinga katika kampeni zake. Aina hiyo ya uchezaji ilimsadia kwa kiasi kikubwa katika michuano hiyo lakini bado haijajulikana kama itaweza kufanya kazi vyema katika Ligi Kuu. Mata aliongeza kuwa kwasasa wanajaribu kucheza katika mfumo huo mpya, hajui muda gani wanaweza kuuuzoea lakini wanafanya kila wanaloweza kuhakikisha wanauzoea na kuamini wanachokifanya.

No comments:

Post a Comment