Saturday, July 26, 2014

NILISHINDWA KUMSAJILI SHAW KWA SABABU YA MSHAHARA - MOURINHO.

MENEJA wa Chelsea, Jose Mourinho amedai alijitoa katika kinyang’anyiro cha kumsajili beki wa kushoto Luke Shaw katika kipindi hiki cha usajili wa kiangazi kwasababu mshahara aliohitaji ungeweza kuivuruga klabu hiyo. Shaw amekuwa beki wa nne ghali zaidi katika historia wakati Manchester United walipomsajili mapema mwezi huu kwa paundi milioni 27 akitokea Southampton. Mourinho amesema Shaw alikuwa akitaka mshahara wa paundi 100,000 kwa wiki ambao amedai ni mkubwa sana kwamchezaji mwenye umri wake wa miaka 19. Kocha huyo alidai kuwa kama wangefanya hivyo wangepunguza morari ya timu kwa kiasi kikubwa kwani kuna wachezaji wengi klabuni hapo ambao wamecheza mechi zaidi ya 200 na kushinda karibu kila kitu lakini hawajafikia kiwango hicho. Mourinho amesema kutokana na sababu hiyo pamoja na kuogopa kukiuka sheria ya matumizi ya fedha ndio mambo yalimfanya kujitoa katika kinyang’anyiro hicho.

No comments:

Post a Comment