Saturday, July 26, 2014

JUVENTUS BADO INAHITAJI KUSAJILI - ALLEGRI.

MENEJA mpya wa klabu ya Juventus, Massimiliano Allegri amethibitisha kuwa anataka kusajili mshambuliaji na beki kabla ya dirisha la usajili majira ya kiangazi halijafungwa. Mabingwa hao wa Italia walikamilisha uhamisho wa winga wa Udinese Roberto Pereyra jana kwa mkopo ikiwa ni siku chache baada ya kuwasajili beki wa kushoto wa Manchester United Patrice Evra na mshambuliaji wa Real Madrid Alvaro Morata. Usajili huo wa wachezaji hao watatu umekuja kufuatia kocha Antonio Conte kujiuzulu ghafla mwiki iliyopita na Allegri ambaye alichukua nafasi yake amebainisha mipango yake ya kuimarisha kikosi hicho kabla ya kuanza kwa msimu mpya. Akihojiwa Allegri amesema kama wakisajili beki mmoja na mshambuliaji kikosi chao kitakuwa katika hali nzuri tayari kwa ajili ya kutetea taji lao la ligi.

No comments:

Post a Comment