Sunday, July 27, 2014

MAN UNITED BADO WAMKOMALIA VERMAELEN.

KLABU ya Manchester United bado imeendelea kuwa na uhakika wa kukamilisha usajili wa Thomas Vermaelen katika kipindi hiki cha majira ya kiangazi pamoja na Barcelona nao kuonyesha nia ya kumtaka beki huyo. United bado hawajafikia makubaliano ya ofa ya kumsajili beki huyo wa kati na Arsenal lakini inaaminika kuwa klabu bado ina nia ya kumsajili pamoja na dau lao la euro milioni kukataliwa. Vermaelen mwenyewe anataka kuondoka Arsenal kiangazi hiki lakini meneja Arsene Wenger anahitaji kusajili mbadala wake kabla ya kuamua kumuuza. United wanaoenekana hawako peke yao katika vita hiyo ya kumsajili Vermaelen kwasababu Barcelona nao bado wanahitaji kusajili beki mwingine baada ya kumnyakua Jeremy Mathieu kutoka Valencia.

No comments:

Post a Comment