Sunday, July 27, 2014

BOLT ATUA GLASGOW TAYARI KWA AJILI YA MASHINDANO YA JUMUIYA YA MADOLA.

MWANARIADHA nyota wa mbio fupi wa Jamaica, Usain Bolt amesema anatarajia kukimbia mbio za kufuzu za mita 400 kupokezana vijiti katika michuano ya Jumuiya ya Madola inayoendelea jijini Glasgow, Scotland. Bolt mshindi wa medali sita za dhahabu katika michuano ya olimpiki, hajashindana katika michuano yoyote kwa mwaka huu na hajawahi kushindana katika michuano ya Jumuiya ya Madola hapo kabla. Lakini mwaka huu Bolt aliowaondoa hofu mashabiki wake baada ya kutua Glasgow jana na kuthibitisha kukimbia mbio za kufuzu kabla ya kuanza safari ya kugombea medali katika mbio hizo za kupokezana vijiti. Mbio hizo za kufuzu zinatarajiwa kufanyika Ijumaa ijayo huko Hampden Park kabla ya fainali zenyewe ambazo ndio itakuwa tukio la mwisho katika michuano hiyo Agosti 2 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment