Sunday, July 27, 2014

JAMES RODRIGUEZ NI HAZINA YA MADRID KWA SIKU ZIJAZO - ANCELOTTI.

MENEJA wa klabu ya Real Madrid, Carlo Ancelotti amesema James Rodriguez ni hazina kwa ajili ya timu hiyo siku zijazo. Kauli ya Ancelotti imekuja kufuatia mchezo wa kirafiki dhidi ya Inter Milan uliofanyika jana ambapo timu hizo zilitoka sare ya kufungana bao 1-1 na kupelekea timu hizo kwenda kwenye hatua ya changamoto ya mikwaju ya penati. Akihojiwa Ancelotti amesema Rodriguez anatarajiwa kuwasili rasmi Agosti mosi na kuongeza kuwa ni mchezaji muhimu na ana uwezo uwezo wa kucheza katika kikosi chake cha kwanza. Ancelotti pia akiri kuwa klabu hiyo kwasasa haina mpango wa kusajili tena mshambuliaji kwasasa tayari wanao wengi wakiwemo Rodriguez na Tony Kroos waliosajiliwa kiangazi hiki. Kocha huyo pia alithibitisha kuwa winga wake Angel Di Maria anakaribia kusajiliwa na klabu ya Paris Saint-Germain.

No comments:

Post a Comment