Sunday, July 27, 2014

WILSHERE AJUTIA NA KUOMBA RADHI KWA KITENDO CHAKE CHA KUVUTA SIGARA.

KIUNGO mahiri wa klabu ya Arsenal Jack Wilshere amekiri na kujutia kitendo chake cha kuvuta sigara katika picha aliyopigwa akiwa katika likizo ya Kombe la Dunia na kusisitiza kuwa atafanya jitihada kuhakikisha anarejea katika kiwango chake bora msimu huu unaokuja. Wilshere alizua utata wakati picha ikimuonyesha akivuta sigara katika bwawa la kuogolea jijini Las Vegas ilipovuja mapema mwezi huu, muda mfupi baada ya Uingereza kutolewa katika michuano ya Kombe la Dunia. Meneja Arsene Wenger amekuwa akiipinga vikali tabia hiyo kwa wachezaji wake na toka wakati huo amefanya nae mazungumzo na nyota huyo mwenye umri wa miaka 22 amekiri hadharani kuwa alifanya tukio hilo na kwamba ni bahati mbaya. Akihojiwa Wilshere amesema anajutia kitendo chake hicho hususani kwa kukirudia kwa mara ya pili na kudai kuwa bado ana umri mdogo hivyo anajifunza kutokana na makosa anayofanya.

No comments:

Post a Comment