Sunday, July 27, 2014

OSPINA ATUA RASMI ARSENAL.

KOCHA wa klabu ya Nice, Claude Puel amedai kuwa Arsenal tayari imekamilisha usajili wa golikipa wa kimataifa wa Colombia David Ospina. Ospina mwenye umri wa miaka 25 amekuwa akiichezea klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu nchini Ufaransa toka mwaka 2008 huku akiisaidia nchi yake kutinga hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Dunia iliyomalizika nchini Brazil hivi karibuni. Kocha wa Arsenal Arsene Wenger naye alithibitisha kumsajili kipa huyo na kusifia kwamba ni usajili mzuri hususani kwa kiwango alichoonyesha golikipa huyo kwa kufanya vizuri katika Kombe la Dunia. Wenger amekuwa katika mawindo ya kutafuta golikipa mwingine atakayempa changamoto Wociech Szczesny katika kugombea nafasi katika kikosi cha kwanza baada ya kuondoka kwa Lukas Fabianski.

No comments:

Post a Comment