Thursday, August 14, 2014

CAS YATUPILIA MBALI RUFANI YA SUAREZ LAKINI WAMRUHUSU KUFANYA MAZOEZI NA BARCELONA.

MAHAKAMA ya Kimataifa ya Usluhishi wa Michezo, CAS imetupilia mbali rufani ya kupunguziwa adhabu ya mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Uruguay Luis Suarez lakini ameruhusiwa kufanya mazoezi na timu yake mpya ya Barcelona. Mawakili wa Suarez walikata rufani CAS kupinga uamuzi wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kumfungia mteja wao miezi minne kujishughulisha na mambo ya michezo kwa kosa la kumng’ata Giorgio Chiellini katika michuano ya Kombe la Dunia. Sasa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 ambaye atamaliza adhabu yake Octoba 25 ataweza kucheza mechi yake ya kwanza katika mchezo wa El Clasico wakati Barcelona watakapokuwa wageni wa Real Madrid Octoba 26 mwaka huu. Nyota huyo pia ataendelea kuitumikia adhabu yake ya mechi tisa za kimataifa kama kawaida lakini sasa masharti yamelegezwa kidogo kwani anaweza kufanya mazoezi na wenzake na pia kuhudhuria mechi.

No comments:

Post a Comment