Friday, August 22, 2014

FIFA YAKOMAA MICHUANO YA KLABU YA DUNIA IFANYIKE MOROCCO PAMOJA NA EBOLA.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA, limethibitisha kuwa michuano ya Klabu Bingwa ya dunia itakayoihusisha Real Madrid itafanyika nchini Morocco kama ilivyopangwa Desemba mwaka huu pamoja na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola ulioathiri nchi kadhaa barani Afrika. Katika taarifa yake FIFA imedai kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani-WHO hakuna mgonjwa yoyote aliyepatikana Morocco hivyo hawaoni sababu ya kubadilisha sehemu. Virusi hivyo hatari vya Ebola tayari vimeua watu wapatao 1,350 katika nchi nne magharibi mwa Afrika zikiwemo Liberia, Guinea, Nigeria na Sierra Leone toka uanza kulipa Machi mwaka huu. Mabingwa wa Ulaya Madrid tayari wamefuzu michuano hiyo itakayoanza Desemba 10 hadi 20 wakiwa sambamba na timu za San Lorenzo kutoka Argentina, Cruz Azal kutoka Mexico, Auckland City kutoka New Zealand na wenyeji Moghreb Tetouan. Mabingwa kutoka bara la Afrika na Asia nao watashiriki michuano hiyo ambapo mwaka jana Bayern Munich ndio walioibuka kidedea katika michuano iliyofanyika hapohapo Morocco.

No comments:

Post a Comment