Friday, August 22, 2014

GALATASARAY YAMPOTEZEA PODOLSKI.

RAIS wa klabu ya Galatasaray amethibitisha kuwa timu hiyo haitatoa ofa yoyote kwa ajili mshambuliaji wa Arsenal, Lkas Podolski. Kumekuwa taarifa wiki hii zinazodai kuwa Arsenal wako tayari kumuuza nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani ambaye ameshindwa kupata namba ya kudumu katika kikosi cha kwanza toka atue katika Uwanja Emirates mwaka 2012. Lakini wakati bosi huyo Galatasaray Unal Aysal akikiri kufanya mazungumzo na meneja wake Cesare Prandelli kuhusu Podolski, amebinisha kuwa kocha huyo amemshauri kuachana na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29. Aysal amesema alimuuliza Prandelli kama anamtaka Podolski lakini alimjibu kuwa huo utakuwa usajili wa kifahari ambao hana shida nao kwa sasa.

No comments:

Post a Comment