Friday, August 22, 2014

SIJUTII FABREGAS KWENDA CHELSEA - WENGER.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amekiri kuwa anaona tofauti anapomuona Cesc Fabregas akiichezea Chelsea katika fulana ya bluu lakini amesisitiza kuwa hajutii kutomsajili tena. Wenger aliwaambia waandishi wa habari kuwa kitu pekee anachojutia ni kuondoka kwa Fabregas mwaka 2011 kwenda Barcelona na kudokeza kuwa bado anataka kusajili kiungo mwingine kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili. Kiungo huyo wa kimataifa wa Hispania mwenye umri wa miaka 27 ambaye amecheza mechi zaidi ya 300 akiwa Arsenal alianza vyema katika timu yake mpya ya Chelsea wakati waliposhinda mabao 3-1 dhidi ya Burnley Jumatatu. Wenger amesema hajutii mchezaji huyo kujiunga na mahasimu wao ingawa anaona tofauti lakini inabidi ukubali kuwa ni kawaida kwa wachezaji wa kulipwa kuhama kutoka klabu moja kwenda nyingine. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa kuondoka kwa Fabregas kulimpa nafasi nyota wa kimataifa wa Wales Aaron Ramsey mwenye umri wa miaka 23 kuibuka katika kikosi chake kwanza.

No comments:

Post a Comment