Friday, August 22, 2014

PATASHIKA LIGI YA MABINGWA AFRIKA KESHO.

MPAMBANO wa kugombea nafasi ya juu ndio jambo la muhimu wakati tukielekea kufunga pazia la hatua ya makundi ya michuano ya Ligi ya mabingwa barani Afrika mwishoni mwa wiki hii. Ingawa nafasi za nusu fainali zikiwa tayari zimejulikana vita iliyobaki sasa ni kujua nani anamaliza katika nafasi juu katika makundi. Timu zilizovuka hatua inayofuata ni AS Vita na TP Mazembe zote za Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo-DRC katika kundi na Entene Setif ya Algeria na CS Sfaxien ya Tunisia katika kundi B. Baada ya kuvuka sasa timu hizo zitakuwa zikigombea nafasi ya kuondoza kundi ambapo Jumapili Mazembe watavaana na mahasimu wao Vita ambao wameshangaza wengi baada ya kupenya katika kundi lililokuwa na timu kongwe kama Zamalek ya Misri na Al Ahly ya sudan. Kesho kutakuwa na mchezo mwingine wa kundi B ambapo Sfaxien wenyewe watakuwa wenyeji wa Setif huku leo kukiwa mchezo wa kundi A kati ya Al Ahly dhidi ya Zamalek. Mechi nyingine ya kundi B itachezwa Jumapili ambapo Esperance ya Tunisia wataivaa Ahly Benghazi ya Libya.

No comments:

Post a Comment