Friday, August 22, 2014

NEWCASTLE YAMUWINDA AYEW.

KLABU ya Newcastle United imeripotiwa kuwa inataka kumsajili kiungo wa kimataifa wa Ghana Andre Ayew. Ayew ameshawahi kukaririwa Mei mwaka huu akidai kuwa na hamu kubwa ya kucheza katika Ligi Kuu ambayo huwa inaangaliwa sana nchini kwao Ghana. Nyota huyo amesema huwa anapenda kila kitu kuhusiana na ligi hiyo, ikiwemo mechi, hali ilivyo, mashabiki na ushindani uliopo. Mabao mawili aliyofunga katika Kombe la Dunia akiwa na Ghana yameonyesha kumuweka juu pamoja na timu yake kushindwa kung’ara katika michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment