Monday, August 25, 2014

HAYATOU ATAKA ADHABU KWA WALIOSABABISHA KIFO CHA MCHEZAJI WA CAMEROON.

RAIS wa Shirikisho la Soka barani Afrika-CAF, Issa Hayatou ameonya kuwa Afrika haitatumika kama chimbuko la utovu wa nidhamu. Hayatou ametoa kauli hiyo baada ya mshambuliaji wa kimataifa wa Cameroon Albert Ebosse anayecheza katika klabu ya JS Kabylie ya Algeria kupigwa na jiwe kichwani na kufariki dunia wakati wa mchezo wa ligi ya nchi hiyo. Hayatou ameagiza hatua kali za kisheria kuchukuliwa ilikukabiliana na utovu wa Usalama. Ebosee mwenye umri wa miaka 24, aligongwa kichwani baada ya timu yake kushindwa mabao 2-1 na USM Alger mjini Tizi Ouzou. Shiriklisho la Soka la Algeria limeagiza kufungwa kwa Uwanja wa 1st Novemba 1954 uliotumika kwa ajili ya mchezo huo. Ebosse alikuwa mfungaji bora msimu uliokamilika akiwa na jumla ya mabao 17 tangu awasili nchini humo kutoka Malaysia.

No comments:

Post a Comment