Friday, August 22, 2014

LIVERPOOL YAMTEGA ETO'O KWA MKATABA WA MWAKA.

KLABU ya Liverpool imemtengea ofa ya mkataba wa mwaka mmoja mshambuliaji wa zamani wa Chelsea Samuel Eto’o ili aweze kutua Anfield. Liverpool ambao wanakaribia kumsajili Mario Balotelli kutoka AC Milan, pia wako tayari kumleta na Eto’o wakati meneja Brendan Rodgers akiwa katika mipango ya kuimarisha safu yake ya ushambuliaji kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili. Eto’o ni mchezaji huru toka alipoondoka Chelsea mapema kiangazi na amekuwa akivivutia vilabu kadhaa barani Ulaya, Amerika na Mashariki ya Kati. Ila nyota huyo wa kimataifa wa Cameroon bado anataka kubakia nchini Uingereza baada ya kucheza kwa mafanikio msimu mmoja akiwa na Chelsea. Vilabu vya Ajax Amsterdam ya Uholanzi na Everton vimeonyesha nia ya kumtaka lakini inaonekana Liverpool sasa ndio wako katika nafasi nzuri ya kumchukua nyota huyo wa zamani wa Barcelona na Inter Milan.

No comments:

Post a Comment