Friday, August 22, 2014

MACKAY AOMBA RADHI.

KOCHA Malky Mackay ameomba radhi kwa ujumbe wa simu aliokuwa akituma na kukiri kuwa haikuwa na maudhui mazuri kwa tamaduni zingine. Kocha huyo wa zamani wa Cardiff City na mfanyakazi mwingine wa zamani wa timu hiyo Iain Moody wanatuhumiwa kutumiana ujumbe wa kudhalilisha matabaka fulani katika jamii ikiwemo masuala ya ubaguzi wa rangi, jinsia na ushoga. Lakini Mackay mwenye umri wa miaka 42 amesema ujumbe aliokuwa akituma ilikuwa ni sehemu ya utani kati yake na rafiki yake Moody. Chama cha makocha wa Ligi nchini Uingereza kilituma taarifa kuwa mackay ameomba radhi kama ujumbe wake ulidhalilisha matabaka mengine. Wawili hao walitimuliwa Cardiff msimu uliopita na klabu hiyo ya Wales wamewashitaki Chama cha Soka cha Uingereza-FA kwa ajili ya hatua zaidi. Moody naye ambaye alikuwa amepata kibarua cha ukurugenzi wa michezo katika klabu ya Crystal Palace alijiuzulu wadhifa wake huo jana lakini hajatoa kauli yoyote kuhusiana na tuhuma hizo.

No comments:

Post a Comment