Thursday, August 28, 2014

MISRI YAJITOSA KINYANG'ANYIRO CHA AFCON.

CHAMA cha Soka nchini Misri nacho kimejitosa katika kinyang’anyiro cha kugombea nafasi ya kuandaa michuano ya Mataifa ya Afrika-Afcon mwaka 2017 baada ya kuandaa michuano hiyo mwaka 2006. Vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoendelea nchini Libya viwalazimisha kujitoa katika mipango ya kujenga viwanja hatua ambayo imelilazimu Shirikisho la Soka Barani Afrika-CAF kutafuta mwenyeji mwingine wa michuano hiyo. Chanzo kimoja cha habari kutoka ndani ya EFA kimebainisha nia ya kutaka kuwa mwenyeji wa michuano hiyo lakini bado hawajafanya uamuzi wa mwisho kuhusiana na suala hilo. Makamu wa rais wa EFA Hassan Farid naye alithibitisha nia yao hiyo lakini amesema bado wanataka kuzungumza na baadhi ya wizara serikalini ili kupata ushirikiano wao. Misri ni mojawpao ya nchi chake barani Afrika zenye miundo mbinu mizuri ya kuandaa michuano mikubwa kama Afcon.

No comments:

Post a Comment