Thursday, August 28, 2014

ROONEY NAHODHA MPYA UINGEREZA.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Manchester United, Wayne Rooney ametajwa kuwa nahodha mpya wa timu ya taifa ya Uingereza na kocha Roy Hodgson. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 amechukua beji hiyo kutoka kwa kiungo wa Liverpool Steven Gerrard ambaye alistaafu rasmi soka la kimataifa baada ya nchi hiyo kutolewa katika michuano ya Kombe la Dunia. Rooney amefunga mabao 40 katika mechi 95 za kimataifa na alitajwa kuwa nahodha wa United na kocha Louis van Gaal mapema mwezi huu. Rooney alithibitisha uteuzi huo katika mtandao wake na kudai kuwa ataitumikia nafasi hiyo kwa bidii na kujivunia huku akidai kuwa zilikuwa ndoto zake za muda mrefu. Rooney ataanza kuvaa beji rasmi akiwa na timu ya taifa Septemba 3 mwaka huu wakati Uingereza watakapoikaribisha Norway katika Uwanja wa Wembley kwa ajili ya mchezao wa kirafiki wa kimataifa.

No comments:

Post a Comment