Friday, August 29, 2014

RONALDO AMTABIRIA MAFANIKIO DI MARIA AKIWA UNITED.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo, amemtabiria mafanikio mchezaji mwenzake wa zamani Angel Di Maria katika klabu yake mpya ya Manchester United. Nyota huyo wa kimataifa wa argentina alifanikiwa kukamilisha usajili uliovunja rekodi nchini Uingereza Jumanne iliyopita baada ya kushindwa kufiti katika kikosi cha Carlo Ancelotti huku akipewa jezi namba saba ambayo imewahi kutimiwa na Ronaldo wakati akiwa United. Ronaldo ambaye alicheza misimu sita na United, anaamini kuwa uhamisho huo ndio Di Maria aliokuwa akihitaji na ana uhakika nyota huyo anaweza kuisaidia timu hiyo kubadili mwelekeo baada ya kuanza vibaya msimu mpya wa Ligi Kuu. Akihojiwa Ronaldo ambaye jana ametunukiwa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka barani Ulaya katika sherehe zilizofanyika jijini Monaco, amesema Di Maria kwenda United ni jambo ambalo litamsaidia kwani anaamini amekwenda katika moja ya klabu bora duniani hivyo anamtakia mafanikio akiwa huko. Ronaldo aliendelea kudai kuwa amezungumza naye na kumwambia kuwa jezi namba aliyopewa ina majukumu makubwa lakini anadhani ataitendea haki jezi hiyo kwani ni mchezaji mahiri.

No comments:

Post a Comment