Thursday, August 28, 2014

SFAXIEN YATAKA MCHEZO WAO WA DRC DHIDI YA VITA URUDIWE.

SHIRIKISHO la Soka la Tunisia-TFT, limetuma barua Shirikisho la Soka la Afrika-CAF kuwataka kuhamisha mchezo wao wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya klabu ya CS Sfaxien na AS Vita nje ya nchi ya jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo-DRC. Sfaxien walifanikiwa kutinga hatua hiyo baada ya kumaliza kama vinara wa kundi B wakati klabu ya Vita wao walimaliza katika nafasi ya pili katika kundi A. Ofisa mkuu wa TFT Shafiq Jarraya amesema wamefikia uamuzi huo wa kuiomba CAF kuhamisha mchezo huo baada ya taarifa za kusambaa kwa virusi vya ugonjwa wa Ebola nchini humo. Jarraya amesema wana matumaini makubwa CAF watakubali maombi yao kwasababu timu itakuwa katika hatari ikienda huko.

No comments:

Post a Comment