Thursday, August 28, 2014

BAYERN YANASA BEKI KUTOKA ROMA.

KLABU ya Bayern Munich imefanikiwa kumsajili beki wa kimataifa wa Morocco Mahdi Benatia kutoka klabu ya AS Roma ya Italia kwa ada ambayo haikuwekwa wazi. Beki huyo mwenye umri wa miaka 27 ambaye aliisaidia Roma kumaliza katika nafasi ya pili katika Serie A msimu uliopita alikuwa akihusishwa pia na tetesi za kutakiwa katika vilabu vua Chelsea na Manchester United. Bayern walikuwa wanatafuta beki baada ya nyota wa kimataifa wa Hispania Javi Hernandez kupata majeraha ya goti yatakayomuweka nje uwanjani mpaka mwakani. Roma tayari wameziba nafasi Benatia kwa kusajili beki wa klabu ya Olympiakos Kostas Manolas.

No comments:

Post a Comment