Thursday, August 28, 2014

PUTIN AZINDUA UWANJA UTAKAOTUMIKA KATIKA YA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA 2018.

RAIS wa Urusi Vladimir Putin jana amefungua uwanja mpya wa Otkrytie uliopo jijini Moscow ambao utatumika kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018. Uwanja huo uliopo kaskazini-magharibi mwa mji mkuu huo, utakuwa ukitumiwa na klabu maarufu ya Spartak Moscow huku ukitarajiwa kutumika kwa baadhi ya mechi katika michuano hiyo. Putin alitua katika uwanja huo kwa helikopta akiwa ameongozana na waziri wa michezo wa Urusi Vitaly Mutko, meya wa jiji la Moscow Sergey Sabyanin na mmiliki wa Spartak ambaye ndiye aliyetoa fedha za ujenzi huo Leonid Fedun. Rais huyo alitembezwa sehemu mbalimbali za uwanja huo ambao kwasasa una uwezo wa kuingiza watazamaji 42,000 huku pia akikutana na wachezaji wakongwe pamoja na chipukizi wa Spartak. Uwanja huo uliochukua miaka saba kutengenezwa umegharimu kiasi cha dola milioni 415 huku pia ukiwa na uwezekano wa kuongezeka na kufikia uweo wa kuingiza watu 45,000.

No comments:

Post a Comment