Thursday, August 28, 2014

FA WANA UHAKIKA WA WEMBLEY KUPATA NAFASI YA KUANDAA FAINALI YA EURO 2020.

CHAMA cha Soka nchini Uingereza, FA kina uhakika kuwa Uwanja wa Wembley una nafasi kuandaa fainali ya michuano ya Ulaya 2020 na pia hawajatoa uwezekano wa kuandaa michuano hiyo mwaka 2028. Katibu Mkuu wa FA Alex horne ana matumaini uwanja huo wa taifa wa Uingereza unaweza kuandaa mchezo wa nusu fainali na fainali katika kipindi cha miaka sita ijayo. Uwanja wa Allianz Arena uliopo jijini Munich ndio uwanja mwingine pekee unaogombani nafasi hiyo na Hornes anafikiri nafasi yao inaongezeka kutokana na Ujerumani kutilia mkazo nafasi yao ya kuandaa michuano ya Ulaya mwaka 2024. Michuano ya Ulaya mwaka 2020 itaandaliwa katika miji 13 tofauti huku mchezo wa fainali na nusu fainali ukiandaliwa katika uwanja mmoja huku miji iliyoshinda kupata nafasi hiyo ikitarajiwa kutangazwa Septemba 19 mwaka huu. Mara ya mwisho Uingereza kuandaa michuano mikubwa ya soka ilikuwa ni mwaka 1996 walipoandaa michuano ya Ulaya huku pia wakiwa wamewahi kuandaa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 1966.

No comments:

Post a Comment