Thursday, August 28, 2014

BAYERN NI BORA KULIKO CHELSEA NA MADRID - ROOBEN.

WINGA wa klabu ya Bayern Munich, Arjen Rooben amesisitiza kuwa klabu yake hiyo ni bora kuliko vikosi alivyowahi kucheza katika vilabu vya Real Madrid na Chelsea. Nyota huyo wa kimataifa wa Uholanzi aliwahi kuvaa jezi za Chelsea kati ya mwaka 2004 na 2007 kabla ya kuondoka na kwenda Santiago Bernabeu na baadae kutua Bayern kipindi cha kiangazi mwaka 2009. Robben amesema hajutii uamuzi wake wa kujiunga na mabingwa hao wa Bundesliga kwani anaamini ndio klabu bora aliyoitumikia katika maisha yake ya soka. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 30 aliendelea kudai kuwa toka ametua katika timu hiyo kiwango kimekuwa kikipanda huku akiamini mambo yataendelea kumnyookea katika siku zijazo pia.

No comments:

Post a Comment