Thursday, September 25, 2014

CAIN HOY YAJITOA KUINUNUA SPURS.

KAMPUNI ya uwekezaji ya Marekani ya Cain Hoy imedai kuwa haifikirii tena kutoa ofa kwa ajili ya kuinunua klabu ya Tottenham Hotspurs. Septemba mwaka huu kampuni hiyo ilithibitisha kuwa iko katika hatua za awali za kupitia ofa kwa ajili ya kuinunua klabu hiyo ya Ligi Kuu. Lakini kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa katika soko la hisa la London, kampuni imedai kusitisha nia yake hiyo. Cain Hoy wana muda mpaka Octoba 10 mwaka huu kuhthibitisha nia yao au kujiondoa rasmi katika kinyang’anyiro hicho. Kwasasa Spurs inajaribu kukusanya fedha kwa ajili ya mpango wa ujenzi wa uwanja mpya utakaokuwa na uwezo wa kuingiza mashabiki 56,250.

No comments:

Post a Comment