Thursday, October 23, 2014

HALI YA SCHUMACHER INATIA MATUMAINI - DAKTARI.

DAKTARI ambaye alikuwa akimtibu Michael Schumacher kwa karibu miezi sita baada ya kupata majeraha ya kichwani katika ajali ya kuteleza katika barafu amesema bingwa huyo wa zamani wa mashindano langalanga anaendelea vyema. Lakini Jean-Francois Payen ambaye ni daktari katika hospitali ya Grenoble ya Ufaransa ambayo Schumacher alitibiwa ameonya kuwa hali yake inaweza kuchukua muda mrefu kidogo wa kati ya mwaka mmoja mpaka mitatu. Schumacher mwenye umri wa miaka 45 alikuwa akiteleza katika barafu katika milima ya Ufaransa Desemba mwaka jana wakati alipoanguka na kugonga kichwa katika jiwe. Dereva huyo huyo bingwa wa langalanga kutoka Ujerumani aliwekwa katika hali ya kutojitambua ili kumsaidia ubongo wake kupona taratibu wakati akipatiwa matibabu Grenoble na baadae kuhamishiwa Lausanne, Switzerland. Schumacher sasa ameshaondolewa hali ya kutojitambua na amekuwa akipata uangalizi wa karibu nyumbani kwake ambapo Profesa Payen amekuwa akimtembelea kufuatilia maendeleo yake.

No comments:

Post a Comment