Thursday, October 23, 2014

KUELEKEA KATIKA MCHEZO WA EL CLASICO KATI YA REAL MADRID NA BARCELONA WAJUE MASTAA NA TIMU WANAZOSHANGILIA.

Jenifer Lopez au J Lo na mwanae wakiwa wametinga jezi za Real Madrid.

Mchezaji tenisi nyota wa Hispania naye ni shabiki namba moja wa Madrid.

Mfalme wa Jordan Abdullah naye ni mnazi wa Madrid, pichani akisalimiana na rais wa klabu hiyo Florentino Perez.

Dogo Justin Bieber naye anaifagilia Barcelona, pichani anaonekana akiwa ametinga jezi ya timu hiyo wakati alipokuwa ziarani Hispania.

Shakira yeye ni zaidi ya mnazi kwani mume wake Gerard Pique ndio kitasa cha kutegemewa Barcelona, picha wakiwa na mtoto wao katika moja ya mechi za timu hiyo.

Mkali wa mpira wa kikapu kutoka NBA katika timu ya Los Angeles Lakers, Kobe Bryant na kafa kaoza kwa Barcelona.

Sio Hollywood pekee bali mpaka Bollywood, pichani ni nyota wa filamu wa India Ranbir Kapoor naye anaishabikia Barcelona.

Mkongwe wa kikapu katika NBA, Magic Johnson pia ni mzee wa Catalan.

No comments:

Post a Comment