Thursday, October 30, 2014

MESSI APIGWA BAO TENA, MASCHERANO ANYAKUWA TUZO YA MCHEZAJI BORA WA MWAKA WA BARCELONA.

KIUNGO mahiri wa Barcelona, Javier Mascherano amechaguliwa kuwa mchezaji wa mwaka wa klabu hiyo na kumshinda nahodha wake wa timu ya taifa ya Argentina na mchezaji bora wa zamani wa dunia Lionel Messi. Mascherano amekuwa akicheza kwa kiwango kikubwa wakati Barcelona wakikabiliwa na msimu mgumu aionyesha uwezo mkubwa wa kumudu nafasi ya beki wa kati na kiungo mkabaji. Messi ameshinda tuzo hiyo mara tatu katika kipindi cha miaka minne lakini amekosa tuzo hiyo ya msimu wa mwaka 2013-2014 kama alivyoikosa tuzo ya mchezaji bora wa dunia wa mwaka aliyochukua Cristiano Ronaldo. 
Mascherano aliwashukuru wale waliompigia kura kushinda tuzo hiyo na kuahidi kuendelea kuonyesha jitihada zaidi kwa msimu mzima. Tuzo hiyo hupigiwa kura na wajumbe maalumu kutoka vyombo vya habari vya Catalan pamoja na maofisa wa juu wa klabu hiyo akiwemo rais wake Josep Maria Bartomeu.

No comments:

Post a Comment