Friday, October 31, 2014

POLISI YAKANUSHA KUKAMATWA KWA MUUAJI WA MEYIWA.

POLISI nchini Afrika Kusini wamekanusha taarifa kuwa watuhumiwa katika kesi ya mauaji ya nahodha wa timu ya taifa ya Afrika Kusini, Bafana Bafana, Senzo Meyiwa wamekamatwa katika daraja la Beit lililopo katika mkapa na Zimbabwe. Msemaji wa jeshi hilo Neville Malila amesema tetesi hizo kuwa kuna mtu amekamatwa sio za kweli ila uchunguzi kuhusiana na tukio hilo bado unaendelea. Mapema kulizuka taarifa kuwa mtuhumiwa mmojawapo wa katika mauaji hayo alikamatwa katika daraja hilo lililopo mpakani na Zimbabwe na kuwa alipelekwa Vosloorus mahali ambako alitenda kosa hilo. Meyiwa aliuawa kwa kupigwa risasi wakati akiwa katika harakati za kumuokoa mpenzi wake Kelly Khumalo nyumbani kwake wakati majambazi walipovamia na kutaka kuwapora vitu vyao vya thamani.

No comments:

Post a Comment