Friday, October 24, 2014

SITAWEZA KUIFUNDISHA BARCELONA - ANCELOTTI.

MENEJA wa klabu ya Real Madrid, Carlo Ancelotti amedai kuwa anaheshimu uhasimu uliopo hivyo hawezi kwenda kuifundisha Barcelona badala yake atastaafu akiwa na hapohapo Santiago Bernabeu. Ni makocha wawili pekee ambao ni Radomir Antic na Enrique Fernandez ambao waliwahi kuzifundisha timu zote hizo mbili kwa nyakati tofauti katika kipindi cha nyuma. Ancelotti ambaye amewahi pia kuzinoa klabu za AC Milan ya Italia na Chelsea ya Uingereza, amesisitiza kuwa kuchukua mikoba ya kuinoa Barcelona ni jambo analiona halitawezekana. Akihojiwa kocha huyo amesema sasa anaifundisha Madrid na kamwe hataweza kuifundisha Barcelona kwasababu anaheshimu historia yake pamoja na historia ya vilabu hivyo. Akiulizwa kama angependa kukaa kwa muda mrefu Madrid kama ilivyokuwa kwa Sir Alex Ferguson katika klabu ya Manchester United, Ancelotti amesema hadhani kama itawezekana kukaa zaidi ya miaka 24 lakini angependa kustaafu akiwa hapo. Madrid wanatofautiana alama nne na Barcelona ambao ndio vinara wa la Liga kuelekea katika mchezo wao huo wa tisa kwa msimu huu.

No comments:

Post a Comment