Friday, October 24, 2014

SERBIA YAPEWA USHINDI WA MEZANI NA UEFA.

SHIRIKISHO la Soka la Ulaya-UEFA limeipa ushindi Serbia wa mabao 3-0 dhidi ya Albania baada ya mchezo wa kufuzu michuano ya Ulaya mwaka 2016 uliofanyika jijini Belgrade kusitishwa kabla ya muda. Lakini pamoja na kupewa ushindi huo, Serbia wamekatwa alama tatu baada ya mchezo huo uliofanyika Octoba 14 mwaka huu kuvunjika wakati ndege isiyokuwa na rubani ilipopita uwanjani huku ikipeperusha bendera iliyokuwa na ujumbe wa kisiasa. Ndege hiyo isiyokuwa na rubani na bendera ilisababisha vurugu kwa mashabiki na rabsha baina ya wachezaji katika Uwanja wa Partizan. Mbali na adhabu hiyo Serbia pia watalazimika kucheza mechi zao mbili za nyumbani bila mashabiki huku vyama vyote vya soka Serbia na Albania vikitozwa faini ya euro 100,000. Nchi zote zimepewa nafasi ya kukata rufani kama hawataridhika na adhabu walizopewa. Serbia sasa wanatarajiwa kucheza mechi zake za kundi I dhidi ya Denmark na Armenia bila mashabiki.

No comments:

Post a Comment